• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP. Posted On: Wednesday, 2nd July 2025

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh Stergomena Lawrence Tax (Mb) amefungua mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF CUP 2025) kwa msimu wa saba tangu kuanzishwa kwake. Ufunguzi huo umefanyika katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi Jijini Dar es Salaam tarehe 02 Julai 2025.

Akizungumza na Maafisa, Askari na wananchi waliohudhuria katika ufunguzi huo amempongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananachi Jenerali Jacob John Mkunda kwa kuendeleza michezo na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt. Samia suhulu Hassan katika kuimarisha sekta ya michezo ambayo kwa sasa ina mchango mkubwa sana kwa Taifa letu.

Naye Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi Luteni Jenerali Salum Haji Othman akimuwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amezitaka timu zote kufuata kanuni na taratibu zinazotawala michezo na kudumisha nidhamu, Kwani kwa kufanya hivyo kutaleta ushindani na kukuza vipaji.

Mashindano haya ya CDF CUP 2025 kwa msimu huu yameboreshwa tofauti na misimu mingine ambapo baadhi ya michezo imeongezwa ambayo ni Kuogelea, karate, Golf, soka la ufukweni, Kuruka vikwazo, Vishale na mieleka.

Mashindano haya yatatamatika tarehe 13 Julai 2025 ambapo Mgeni rasmi wakati wa kufunga mashindano anatarajiwa kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi Jenerali Jacob John Mkunda.

Mashindano haya yatafanyika katika viwanja vya Azam complex kwa mpira wa miguu, Kambi ya Jeshi Twalipo kwa mpira wa wavu, Pete, Kikapu na Mikono (Handball), Mbweni Jkt utachezwa mchezo wa Soka la ufukweni, Msasani utachezwa mchezo wa Vishale, Uwanja wa Golf Lugalo utachezwa mchezo wa golf na Kigamboni (Kamandi ya Jeshi la Wanamaji) utafanyika mchezo wa kuogelea.

Habari Mpya

  • Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    tokea masaa 18
  • ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    tokea siku 4
  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 3
  • Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.