• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Waziri wa Ulinzi na JKT aitembelea Makao Makuu ya Jeshi

Waziri wa Ulinzi na JKT aitembelea Makao Makuu ya Jeshi Posted On: Tuesday, 28th September 2021

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) amefanya ziara Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) yaliyopo Msalato jijini Dodoma kwa lengo la kujitambulisha kwa Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma wanaofanyia kazi Makao Makuu ya Jeshi hilo.

Mhe. Waziri alipokelewa kwa gwaride la heshima na baadae kufanya ukaguzi kabla ya kuambatana na mwenyeji wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo kuelekea ofisini kwake.

Aidha, Mhe. Waziri alipata nafasi ya kusalimiana na Wajumbe wa Kamati Kuu ya Utendaji, Wakuu wa Kamandi na Matawi wakiongozwa na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali Edward Mathew Mkingule.

Baada ya mapokezi hayo Mhe. Waziri alipata wasaa wa kuzungumza mambo mbalimbali na viongozi hao wa ngazi ya juu na baadae kukutana na kada nyingine na kufanya nao mazungumzo.

Mhe. Waziri alisisitiza suala zima la ushirikiano baina ya Jeshi na Wizara kwani kwa kufanya hivyo Jeshi na Wizara kwa pamoja watafikia malengo kwa kuzitafutia ufumbuzi wa pamoja changamoto zitakazokuwa zikijitokeza.

"Mimi ni mtu wa kutunga sera lakini ninyi ndio wataalamu katika utekelezaji wa majukumu yenu ya kila siku. Hivyo basi, tukiunganisha nguvu zetu kwa pamoja tutaweza kuzitatua changamoto zinazojitokeza kwa haraka na kwa usahihi" alisema Mhe. Waziri

Ziara hiyo ya Mhe. Waziri itaendelea kwa kutembeleaKamandi, Brigedi, Vikosi, Vyuo pamoja na Shule kwa lengo la kujitambulisha, kujionea utayari wa kiutendaji wa Jeshi hilo na kuzungumza na watendaji.

Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb), tarehe 10 Septemba, 2021 aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa Mbunge na baadae kuteuliwa tena tarehe 13 Septemba, 2021 kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) akiwa Mwanamke wa Kwanza nchini kushika nafasi hiyo tangu nchi ipate Uhurumwaka 1961.

Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb), anachukua nafasi ya aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Hayati John Elias Kwandikwa.

Kabla ya uteuzi wake wa kuwa Mbunge, Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax, amewahi kuhudumu katika Taasisi mbalimbali ikiwemo Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Habari Mpya

  • Rais Samia Suluhu Hassan atunuku Kamisheni

    Rais Samia Suluhu Hassan atunuku Kamisheni

    tokea miezi 2
  • Waziri Mhe. Bashungwa atembelea zoezi Dragon Fly

    Waziri Mhe. Bashungwa atembelea zoezi Dragon Fly

    tokea miezi 3
  • Zoezi Dragon Fly lafunguliwa

    Zoezi Dragon Fly lafunguliwa

    tokea miezi 3
  • Jenerali Mkunda atembelea Vikosi vya Jeshi Kanda ya Arusha

    Jenerali Mkunda atembelea Vikosi vya Jeshi Kanda ya Arusha

    tokea miezi 3
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 6
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 6
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 6
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miezi 4
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.