• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Waziri wa Ulinzi na JKT Dkt Hussein Mwinyi ziarani Mkoani Mtwara

Waziri wa Ulinzi na JKT  Dkt Hussein Mwinyi ziarani Mkoani Mtwara Posted On: Monday, 19th November 2018

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT ) Dkt Hussein Mwinyi (MB) leo amewasili rasmi Mkoani Mtwara katika moja ya ziara yake kuona maendeleo ya Operesheni Korosho ambayo inasimamiwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.

Aidha Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Yakubu Mohamed, akiambatana na Msimamizi Mkuu wa Operesheni hiyo, Meja Jenerali George Msongole pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evodi Manda walimkaribisha Waziri Dkt Hussein Mwinyi katika kiwanja cha ndege cha Mtwara na kuanza ziara ya kutembelea maeneo ambayo Operesheni Korosho inaendelea katika maeneo tajwa.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Opereshen Korosho Kanali Benjamin Kisinda alisema kuwa zoezi la ubebaji korosho limeshaanza kwa kuhamisha korosho hizo kutoka katika Maghala yaliyokwisha jaa na kuzipeleka katika maghala elekezi ili kupisha upokeaji wa korosho kutoka katika vyama vya wakulima.

Pia Kanali Kisinda alisema kuwa usafirishaji huo umezingatia zaidi maeneo ambayo maghala yamekwisha jaa na barabara zake sio kiwango cha lami zikiwemo Wilaya za Tandahimba, Newala, Masasi, Nachingwea na Liwale.

Habari Mpya

  • ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    tokea siku 3
  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 3
  • Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    tokea mwezi 1
  • Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano

    Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.