Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mh. Dkt. Hussein Mwinyi akabidhiwa ukuta wenye urefu wa kilomita 14.4, unaozunguka uwanja wa ndegevita ulioko Ngerengere Mkoani Morogoro leo tarehe 20 Agosti, 2018.
Sherehe za makabidhiano hayo zilifanyika katika kikosi cha Ndegevita kilichopo Ngerengere. Akizungumza katika uzinduzi huo Waziri Mwinyi ametaka ukuta huo kutunzwa kwani utawasaidia makamanda kulinda miundombinu kambini pamoja na kutekeleza majukumu yao kwa usalama.
Baada ya kuupokea ukuta huo, Dkt. Hussein Mwinyi aliukabidhi rasmi kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ). Kamandi ya Anga.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 9203 Dar es Salaam,
Street :Magore, Upanga
Fax : +255 22 2153432
Tel : +255 22 2150592- 4
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.