Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 21 Agosti, 2021 amempandisha cheo Meja Jenerali Mathew Edward Mkingule kuwa Luteni Jenerali na kumteua kuwa Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania.
Luteni Jenerali Mathew Mkingule anachukua nafasi ya aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa Majeshi hayo, Luteni Jenerali Yacoub Hassan Mohamed aliyeteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uturuki. Kabla ya uteuzi huo Luteni Jenerali Mathew Mkingule alikuwa Mkuu wa Tawi la Udhibiti Fedha Jeshini.
Sambamba na uteuzi huo, pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan aliwaapisha Mabalozi wateule akiwemo Luteni Jenerali Yacoub Mohamed.
Hafla hiyo ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.