Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Methew Mkingule kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo, tarehe 27 Aprili, 2022 ametoa salamu za rambirambi kwa Wakenya wote kwa kufiwa na Rais mstaafu wa Awamu ya tatu, Mhe. Mwai Kibaki aliyefariki hivi karibuni.
Luteni Jenerali Mkingule alifika katika Ubalozi wa Kenya hapa nchini uliopo Jijini Dar es Salaam na kusaini kitabu cha maombolezo kilichopo Ubalozini hapo.
Mnadhimu Mkuu kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF), Maafisa na Askari wa JWTZ alitoa pole kwa Wanajeshi na raia wa Kenya kwa kufiwa na kiongozi huyo.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.