Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Marekani leo Januari 28, 2022. Yamefungua zoezi la pamoja kwa Maafisa na Askari wa vikundi maalum wa majeshi hayo. Zoezi hilo limefunguliwa katika Kituo cha Ulinzi wa Amani Tanzania kilichopo Kunduchi Jijini Dar es Salaam. Aidha, Zoezi hilo litafanyika kuanzia Januari 28, 2022 hadi Machi 18, 2022.
Akizungunza wakati wa ufunguzi wa zoezi hilo, Brigedia Jenerali Idd Said Nkambi amesema, mazoezi kama haya husaidia kubadilishana uzoefu hivyo kuwajengea uwezo Maafisa na Askari katika utekelezaji wa majuku yao. Vile vile mazoezi ya pamoja hujenga uhusiano Mzuri kati ya washiriki na nchi husika kwa ujumla.
Kufanyika kwa zoezi la pamoja kati ya wanajeshi wa Tanzania na wanajeshi wa Marekeni kunaonesha uhusiano thabiti kati ya majeshi hayo.Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.