• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

​JWTZ Yahitimisha Mafunzo ya Soka la Ufukweni

​JWTZ Yahitimisha Mafunzo ya Soka la Ufukweni Posted On: Friday, 14th March 2025

Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Brigedia Jenerali Simon Pigapiga amefunga rasmi mafunzo ya Mchezo wa Soka la Ufukweni yaliyoendeshwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa Wanajeshi wa JWTZ Katika Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa Mbweni leo tarehe 14 Machi 25.

Akimwakilisha Mkuu wa Utumishi Jeshini Meja Jenerali Marco Gaguti, Brigedia Jenerali Pigapiga amewataka wahitimu wa mchezo huo kutumia mafunzo hayo kwa kuwafunza Maafisa na Askari wengine wa JWTZ ili mchezo huo uwe na tija katika mashindano mbalimbali Jeshini.

Aidha, Brigedia Jenerali Pigapiga ameshukuru Uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini kwa usimamizi wa mafunzo hayo.

Akizungumza kwa niaba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu(TFF), Rais wa Shirikisho Bw. Wallace Karia, amesema, Tff inaendelea kushirikiana na JWTZ katika kukuza na kuinua mchezo wa soka nchini, na kuwaomba wahitimu wa mafunzo haya kutumia elimu na maarifa ya mchezo wa Soka la Ufukweni kuwafunza maafisa na Askari katika maeneo wanayotoka. Pia, Bw. Karia amemshukuru Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda kwa kupokea wazo la kuanzishwa mchezo wa Soka la Ufukweni kwani unaonekana kuwa na manufaa kwa jeshi na taifa kwa ujumla.

Mafunzo ya Mchezo wa Soka la Ufukweni kwa Maafisa na Askari wa JWTZ umewezesha jeshi kuwa na wachezaji na wakufunzi wa mchezo huo ambao watatumika kuunda timu katika jeshi na kuunda timu ya taifa chini ya Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), huku miundombinu ya mchezo huo iliyopo katika Kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa Mbweni, ikionekana kuendelea kuimarika, na ujenzi unaendelea.

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa kushirikiana na Shirikisho la mpira wa miguu nchini limedhamiria kuukuza na kuendeleza mchezo wa Soka la Ufukweni kwa kuandaa wachezaji wanajeshi watakaoweza kuitumikia timu ya taifa ya Soka la Ufukweni katika michuano mbalimbali ndani na nje ya bara la Afrika.

Habari Mpya

  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 2
  • Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    tokea wiki 3
  • Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano

    Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

    tokea mwezi 1
  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.