Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda amefunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa Askari wapya wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kundi la 41/22 katika Shule ya Mafunzo ya awali ya kijeshi Kihangaiko kwa Gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake.
Mara baada ya kukagua Gwaride, Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda aliwaasa Askari wapya kuishi kwa kuzingatia viapo vyao vya utii kwani ndio msingi katika kutimiza majukumu yao mapya ya kulilinda taifa la Tanzania.
Aidha, Jenerali Mkunda amewataka Askari wapya kutunza afya zao, pamoja na kuendelea kufanya mafunzo na mazoezi ili kuwa na utayari wakati wowote.
Sherehe za ufungwaji wa kozi hiyo zimepambwa na maonesho mbalimbali ya utendaji kivita, kuruka vikwazo, matumizi ya silaha pamoja na kujilinda dhidi ya adui.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.