Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeaga rasmi Mwili wa Marehemu Meja Jenerali Joseph Lesulie (mstaafu) leo tarehe17 Agosti, 2018 katika Hospitali Kuu ya Jeshi, Lugalo.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akiambatana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo, amewaongoza Makamanda wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Maafisa, Askari na Wananchi kwa ujumla wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu..
Marehemu amezikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.