Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Daniel Baran Sillo amefungua kikao cha Wakuu wa Viwanda na Mashirika ya Kijeshi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) leo tarehe 25 Februari 2025 katika ukumbi wa Twiga Hotel uliopo jijini Dar es salaam.
Kikao hicho ni mwendelezo wa vikao vya kila mwaka, lengo likiwa ni kubadilishana ujuzi hasa katika teknolojia ili kuwa na viwanda vitakavyoweza kufanya vizuri katika uzalishaji kimataifa.
Nchi zinazoshiriki kikao hicho ni pamoja na Kenya, Tanzania, Rwanda, Uganda, Burundi, Somalia pamoja na Sudan ya Kusini ambapo Tanzania ni Mwenyeji wa kikao hicho.
Kikao hicho kinafanyika kwa siku mbili hadi kilele chake tarehe 26 Februari 2025
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.