Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Venance Mabeyo ametembelea na kuzungumza na Maafisa na Askari wa Kanda ya Mwanza tarehe 8 Februari 2021.
Akizungumza na Maafisa na Askari wa Kanda hiyo, Mkuu wa Majeshi amesisitiza umuhimu wa kudumisha nidhamu katika utendaji kazi na pia kuzingatia kiapo cha utii kwa mwanajeshi kwani ndicho kinachotuongoza kwenye majukumu yetu ya kila siku.
Kabla ya kikao hicho Jenerali Mabeyo alitembelea vikosi mbalimbali vilivyopo katika kanda hiyo na kujionea utendaji kazi wa vikosi hivyo.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 9203 Dar es Salaam,
Street :Magore, Upanga
Fax : +255 22 2153432
Tel : +255 22 2150592- 4
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.