• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Majeshi ya Ulinzi wa nchi za Falme za Kiarabu afanya ziara ya kikazi nchini Tanzania

Majeshi ya Ulinzi wa nchi za Falme za Kiarabu afanya ziara ya kikazi nchini Tanzania Posted On: Tuesday, 15th July 2025

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa nchi za Falme za Kiarabu, Luteni Jenerali Eisa Saif Mohamed Bin Ablan Almazrouei amefanya ziara ya kikazi nchini Tanzania leo tarehe 14 Julai 2025.

Jenerali Almazrouei alipokelewa na mwenyeji wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda.

Mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga Jijini Dar es Salaam, Luteni Jenerali Almazrouei alipokea salamu ya heshima na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake.

Wakati wa mazungumzo yake mafupi na ujumbe huo toka Falme za Kiarabu ofisini kwake Upanga, Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda alieleza umuhimu wa ushirikiano wa Kijeshi uliopo baina ya Mataifa haya mawili kuwa unaendelea kudumishwa.

Jenerali Mkunda amesema JWTZ linajivunia, ushirikiano uliopo katika kukabiliana na matishio ya kiusalama kama vile ugaidi na usafirishaji haramu wa binadamu katika nchi mbili hizi. Aidha, maeneo mengine ya ushirikiano ni pamoja na Mafunzo, Utafiti, Utamaduni na Michezo, na kuimarisha ulinzi wa mipaka.

Aidha, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa UAE Luteni Jenerali Almazrouei ameshukuru ukarimu alioneshwa na mwenyeji wake Jenerali Jacob Mkunda na kusisitiza kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya Majeshi haya mawili.

Luteni Jenerali Almazrouei yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya kudumisha ushirikiano uliopo baina ya majeshi haya mawili.

Habari Mpya

  • Majeshi ya Ulinzi wa nchi za Falme za Kiarabu afanya ziara ya kikazi nchini Tanzania

    Majeshi ya Ulinzi wa nchi za Falme za Kiarabu afanya ziara ya kikazi nchini Tanzania

    tokea masaa 20
  • JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    tokea wiki 1
  • Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    tokea wiki 1
  • ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.