Rais na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dokta Samia Suluhu Hassan amewaongoza Watanzania katika Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mashujaa yaliyofanyika viwanja vya Mashujaa Mtumba Jijini Dodoma.
Katika maadhimisho hayo Rais na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dokta Samia Suluhu Hassan ameweka Mkuki na Ngao kwenye Mnara wa Mashujaa ikiwa ni ishara ya kuwaenzi Mashujaa wa nchi hii.
Mbali na Rais na Amiri Jeshi Mkuu kuweka Mkuki na Ngao pia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda aliweka Sime ikiwa ni ishara ya kuwaenzi Mashujaa wa Tanzania.
Maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa hufanyika kila tarehe 25 Julai ya kila Mwaka ikiwa ni kuwaenzi Mashujaa waliomwaga damu kwa ajili ya taifa lao.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.