Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan ametunuku Kamisheni Maafisa Wanafunzi 740 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika sherehe zilizofanyika kwenye Chuo cha Kijeshi cha Maafisa Monduli, Jijini Arusha tarehe 26 Novemba 2022.
Kati ya Maafisa hao wapya, wapo Maafisa waliofanya kozi ya Miaka Mitatu (BMS) 03/2022 pamoja na Maafisa waliofanya kozi ndefu ya mwaka mmoja intake 69.
Mkuu wa Chuo cha Kijeshi Monduli Brigedia Jenerali Jackson Jairos Mwaseba amesema Maafisa hao wapya waliotunukiwa Kamisheni wamefanya mafunzo yao hapa nchini na nje ya nchi wakiwemo waliofanyia mafunzo Nchini China na Urusi.
Mbali na kutunuku Kamisheni, Rais na Amiri Jeshi Mkuu amewatunuku Shahada ya Kwanza ya Sayansi ya Kijeshi Maafisa wapya 109.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.