Rais wa Malawi Dkt. Lazarus Chakwera leo tarehe 07 Oktoba 2020 amefanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini ambapo amepokelewa na mwenyeji wake Dkt. John Pombe Magufuli katika Kiwanja cha ndege cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kupigiwa mizinga 21 pamoja na kukagua gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.
Wakati wa ziara hiyo, Rais huyo atatembelea kituo kipya cha Mabasi yaendayo Mikoani kinachojengwa eneo la Mbezi na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa kituo hicho. Aidha, atatembelea pia bandari ya Dar es Salaam na kujionea namna inavyofanya kazi. Katika ziara hiyo Rais Dkt. Lazarus Chakwera ameambatana na viongozi wengine wa Serikali yake.
Hii ni ziara yake ya kwanza tangu aingie madarakani ikiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano na uhusiano baina ya nchi hizi mbili. Ikumbukwe kuwa Rais Chakwera ameingia madarakani mwezi Juni mwaka huu akipokea kijiti cha uongozi kutoka kwa mtangulizi wake Dkt. Bingu wa Mutharika.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.