Kampuni ya Kimataifa ya Simba International ya Afrika Kusini leo tarehe 17 Disemba, 2020 imemkabidhi Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhandisi Elias John Kwandikwa Hanga la kuhifadhia, kutengezea na mafunzo ya Helikopta za Kijeshi.
Makabidhiano hayo yamefanyika katika Kikosi cha Ndege za Usafirishaji kilichopo Ukonga jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Waziri Kwandikwa aliitaka Kamandi ya Anga kuendelea kuvitunza vifaa na miundombinu mingine iliyopo chini ya Kamandi ili viweze kudumu kwa muda mrefu, kuleta tija na ufanisi katika utendaji wa kila siku.
Kwa upande wake Mkuu wa Majeshi aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuliimarisha Jeshi kwa kulipatia vifaa na zana mbalimbali kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake wakati wote.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.