Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Elias Kwandikwa ametiliana saini na Balozi wa Ujerumani nchini Dkt. Regina Hess Mkataba wa Ujenzi wa Hospitali ya Kijeshi Jijini Dodoma tarehe 18 Februari 2021.
Akiongea kwa niaba ya Serikali, Waziri Kwandikwa aliishukuru Serikali ya Ujerumani Kupitia kwa Ubalozi wake Nchini kwa kudhamini Mradi huo wenye maslahi kwa Jeshi na Taifa.
Kabla ya Kutiliana saini Mkataba huo, pande zote zilitembelea Kituo cha Magonjwa ya kuambukiza katika Hospitali Kuu ya Jeshi, Lugalo Jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia Kituo cha Magonjwa ya Kuambukiza, Balozi Regina alisema kituo hicho cha Afya kimegharimu Sh. Bilioni 21 na kitasaidia kuwatibu wagonjwa wa magonjwa ya Milipuko.
Kwa Upande wake Kamanda wa Kikosi cha GAFTAG Luteni Kanali Thomas Nolbash alisema licha ya Bajeti kuwa finyu lakini watahakikisha mradi wa Hospitali ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Jijini Dodoma anakamilika kwa viwango na wakati.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.