Ujumbe kutoka Jeshi la Jamhuri ya Watu wa China ukiongozwa na Naibu Mnadhimu Mkuu Real Admiral Guan Bailin uliowasili na meli maalum ya matibabu nchini Novemba 19, 2017 leo Novemba 22 umemtembelea Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo na kufanya mazungumzo ofisini kwake.
Ugeni huo bado upo nchini kwa lengo la kutoa huduma ya afya bure kwa wananchi wa Tanzania. Huduma hizo zinatolewa ndani ya meli hiyo na madaktari kutoka China kwa kushirikiana na Madaktari wetu.
Leo ni siku ya nne tangu timu hiyo ya Madaktari kutoka China kutoa huduma na watanzania wameitikia wito.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.