Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax amevitaka vyombo vya Ulinzi na Usalama kushirikiana ili kuilinda nchi ya Tanzania.
Ameyasema hayo kwenye sherehe ya kumuaga aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venancy Salvatory Mabeyo iliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Amesema nchi ya Tanzania itakuwa salama iwapo vyombo vya Ulinzi na Usalama vitashirikiana kikamilifu.
Sherehe hiyo iliandaliwa na Kamati ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa ajili ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti wake Jenerali Venancy Salvatory Mabeyo (Mstaafu) Msasani Klabu Jijini Dar es Salaam.Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.