Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe Dokta Stergomena Lawrance Tax amesisitiza umuhimu wa mafunzo maalum ya kijeshi ili kuwa na jeshi imara katika kulinda mipaka ya nchi.
Ameyasema hayo wakati wa kufunga mafunzo maalum yaliyofanyika kwa ushirikiano kati ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na Jeshi la Watu wa China yaliyofanyika Mapinga mkoani Pwani.
Amesema dunia ya sasa inahitaji ulinzi wenye weledi na ushirikiano wa kimataifa hivyo mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka.
Naye Balozi wa China nchini Tanzania Mhe Chen Mingjian ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa kuyakubali mafunzo maalum ya kijeshi kati ya JWTZ na Jeshi la Watu wa China.
Amesema China na Tanzania zimekuwa na ushirikiano wa kidiplomasia kwa muda mrefu jambo ambalo limeongeza maelewano katika nyanja mbalimbali za mafunzo ya kijeshi
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.